top of page

Korea Kaskazini: Vikwazo vipya ni kama vita

  • Khalidi
  • Dec 24, 2017
  • 1 min read

Korea Kaskazini imetaja vikwazo vya hivi majuzi vya Umoja wa Mataifa dhidi yake ni kama vita.

Wizara ya mashauri ya nchi za kigeni ilisema kuwa hatua hizo zilikuwa ni kubwa na ngumu kwa uchumi kwa mujibu wa shirika la KNCA la Korea Kaskazini.

Iliongeza kuwa kuwa kuongeza msimamo mkali zaidi wa Korea Kaskazini ndilo jibu kwa Marekani.

Baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa lilitangaza vikwazo vipya siku ya Ijumaa kufuatia majaribio ya makombora ya masafa marefu ya Korea Kaskazini.

Marekani ilipendekeza vikwazo hivyo na kuungwa mkono na wanacha wote 15 wa baraza la usalama la Umoja Mataifa vikiwemo vya kukata mauzo ya mafuta kwa asilimia 90 kwa Korea Kaskazini.

Korea Kaskazini tayari iko chini ya vikwani kutoka Marekani, Umoja wa Mataifa na EU


 
 
 

Comments


Top Stories

Join our mailing list

Never miss an update

© 2017 Fahari News 

bottom of page